Saturday, November 24, 2012

KONGAMANO LA CHANGAMOTO ZINAZOKABILI MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU NA ATHARI ZAKE LAFANYIKA CHUO KIKUU MZUMBE

Kongamano hilo la aina yake lililojumuisha wageni kutoka vyuo vikuu mbalimbali (SUA, MOROGORO UNIVERSITY, RUCO na ST. JOSEPH) waliolikwa katika kongamano hilo kubwa kuwahi kutokea vyuoni liliendeshwa na Profesa Mchome (katibu Mkuu wa TCU) kwa kushilikiana na Ndugu Onesmas Laizer (Mwakilishi kutoka Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu) kwa kuwasilisha mada mbalimbali zilizolenga kujadili changamoto zinazoikabili bodi ya mikopo katika utoaji na urejeshwaji wa mikopo na mstakabali wa changamoto hizo. 

Mada nyingi zimejadiliwa ila mada zilizoonekana kutawala mjadala huo ni pamoja na ucheleweshwaji wa mikopo hususani chuo Kikuu Mzumbe, utoaji wa mikopo kwa upendeleo hususani wanafunzi wanaosoma kozi za sayansi jambo linalosababisha baadhi ya wanafunzi kupata mikopo pasipo stahili, mfano baadhi ya wanafunzi wanaofaulu masomo ya sayansi ni wale waliosoma Shule nzuri kama Fedha, St. Marian nk. kuwa wanafunzi hawa wazazi wao wanakuwa na Uwezo wa kuwasomesha, Sera ya vipaumbele "Priorities" kwa baadhi ya kozi kujenga madaraja kwani wanaokimbilia mikopo ni watoto wa masikini ambao hulazimika kusoma kozi ambazo siyo chaguo lao na malipo ya "field studies kucheleweshwa na kutolipwa kwa viwango sahihi.

Akijibu hoja hizo Ndugu Laizer amesema kuwa suala la upendeleo si kweli ni fikra tu zilizojengeka miongoni mwa watu na wanafunzi kwani mikopo hiyo hutolewa kwa kuzingatia taarifa zilizojazwa na Mwanafunzi, kuhusu ucheleweshaji ameahidi kuwa maboresho yanaendelea ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa kunakuwa na mawasiliano ya karibu na vyuo ili kuwahisha matokeo ya wanafunzi mapema  na kuwa suala hilo litabaki kuwa historia tu. kwa upande mwingine amekiri na kumesema kuwa suala hilo inawezekana lipo japo si makosa ya bodi kwani wanaamini kuwa taarifa zinazowafikia bodi zinakuwa ni sahihi kwani zinapitia kwa watenadaji wa vijiji na mitaa wanowafahamu watu. Suala la malipo ya "field studies" hutegemea na asilimia ya mkopo anaoupata mtu, hivyo kutofautiana ni jambo la kawaida.

Aidha mapendekezo yametolewa juu ya uboreshaji, mapendekezo hayo ni pamoja na uongozi wa bodi kufanya ufuatiliaji wa karibu katika taarifa zinazojazwa na wanafunzi ili kuwabaini wadanganyifu pia kufuatilia wanafunzi wanaomaliza vyuo na kuhakikisha mikopo inarudi ili kuwawezesha wanafunzi walioko vyuo kutopata matatizo ya mikopo. Mapendekezo mengine yalikuwa ni kupunguza gharama za kutuma maombi ili kuwawezesha wazazi wa kipato cha chini kumudu gharama hizo na kubadilisha mfumo unaotumika wa sasa wa kutuma maombi kwa njia ya mtandao.

Akihitimisha Kongamano hilo Profesa Itika (Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo) amewashukulu Viongozi  (kutoka TCU, HESLB na NACTE) waliohudhuria kongamano hilo na Serikali ya wanafunzi kwa ujumla.

PICHA KATIKA MATUKIO 

Ndugu Onesmas Laizer akichokoza mada katika Kongamano la Changamoto  zinazowakabili  wanafunzi wa elimu ya juu na athari zake.

Mh. Hamis Mbawala (Waziri wa Wizara ya Mikopo) Serikali ya wanafunzi Mzumbe (MUSO) akitoa maonii.


Kutoka kushoto ni Rais wa Serikali ya wanafunnzi Chuo kikuu mzumbe (MUSO), Kaimu Mkuu wa Chuo kikuu Mzumbo, Profesa Mchome (Katibu Mkuu TCU) na Katibu Mkuu wa NACTE wakifurahia jambo wakati mwakilishi kutoka bodi ya Mikopo akiwasilisha mada.



1 comment:

  1. najiuliza sana maswali kwanini nyie mnaweka mambo yenu hadharani na serikali za wanafunzi wa vyuo vingine wanaficha amuoni kuwa mna kazi kubwa kuwashawishi nao waweke hadharani maana ubadhirifu unaanzia hapo

    ReplyDelete

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

IDADI YA WASOMAJI

RedEnvelope
. .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...