Thursday, November 29, 2012

MAKAMU MKUU WA CHUO KIKUU MZUMBE AFANYA MKUTANO NA WANACHUO!


Makamu Mkuu wa Chuo (Profesa Kuzilwa) amefanya mkutano na wanachuo wa Chuo Kikuu mzumbe "main compas". Mkutano huo ambao umehudhuliwa na wanachuo wengi kiasi cha kuutapisha ukumbi wa mikutano hali ambayo imesababisha baadhi ya wanachuo kukosa nafasi za kukaa umefanyikia katika ukumbi wa mikutano wa chuo ali maarufu NAH yaani "New Assembly Hall" kuanzia majira ya saa  8:00 mchana hadi saa 11:00 jioni.

Katika mkutano huo Makamu Mkuu wa Chuo amezungumzia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Maendeleo ya Chuo kwa ujumla katika masuala ya Taaluma, upanuzi wa miundombinu ya Chuo kama vile ujenzi wa bweni la Maria Nyerere (Mzumbe) mradi ambao umekwishakamilika na ujenzi wa Maktaba katika matawi ya Dar Es Salaam na Mbeya ambao unaendelea kwa sasa na mpango wa ujenzi wa madarasa na hostel kwa Main compas ambao upo kwenye dira ya miaka mitano kuanzia mwaka 2012-2017 baada ya dira ya mwaka 2007-2012 kukamilika kwa mafanikio makubwa.

Akiendelea na hotuba yake ambayo iliyoonekana kuvuta hisia za wanachuo ambao walikuwa na kiu kubwa na shauku ya kutaka kujua mambo mengi alielezea juu ya sheria mpya za mitihani ambazo zimeanza kutumika mwaka wa masomo 2012/2013. Ujio wa sheria hizo mpya umepokelewa kwa furaha kubwa. Suala lingine, aliloligusia ni pamoja na kucheleweshewa mikopo wanafunzi waliokuwa "Stagard semister" alisema kuwa ni sababu za kiufundi ndiyo zilizopelekea mikopo hiyo kuchelewa kwani hata yeye binafsi alikiri kufuatilia suala hilo bodi ya Mikopo.

Mambo mengine aliyoyagusia ni pamoja na kuwaasa wanachuo kutokuendesha siasa au kujihusisha  na shughuli za siasa wawapo chuoni kwani ni kinyume na sheria na 51 (1) ya Chuo Kikuu Mzumbe inayozuia uendeshaji wa shughuli za siasa ndani ya chuo. Pia amewaambia wanachuo kuwa "TCU" imetoa fursa kwa wanafunzi wanaohitaji kusoma baadhi ya mihula au kuhamia katika vyuo vingine kufuatilia maelekezo kwenye mtandao wa "TCU" kwani ni jambo linalowezekana kwa sasa. Kwa mfano, Mwanachuo anaweza kusoma muhula mmoja chuo Kikuu Mzumbe na akaenda kusoma Chuo Kikuu Dar Es Salaam Mhula unaofuata na akarudi kuendelea na masomo yake kama kawaida.

Wanachuo nao walipata fursa ya kuuliza maswali na kutoa maoni yao. Maswali mbalimbali yaliyoulizwa ni pamoja na kuwa kwanini wanachuo wanaokata rufaa ya Mitihani "appeals" wasirudishiwe karatasi za majibu, Makamu Mkuu wa Chuo, akijibu swali hilo, alisema ni jambo ambalo haliko kwenye utaratibu na kuwa haliwezekani. Swali lingine lilikuwa ni kuhusu magari ya abiria kuruhusiwa kuingia Chuoni ili kupunguza usumbufu wanaoupata wanachuo wa kutembea umbali mrefu kutoka na kwenda kituo cha magari, akijibu, Makamu Mkuu wa Chuo alisema hilo linawezekana na litafanyiwa kazi. Katika Swali la kutopewa muda wa michezo katika ratiba na ukosefu wa viwanja vya kutosha kwa ajili ya michezo nalo liliulizwa,  Makamu Mkuu wa Chuo akijibu, amesema kuwa suala la ratiba ni ufuatiliaji, nalo pia lingepatiwa ufumbuzi kwa kumshirikisha Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma (DVC A) na kuhusu viwanja, alisema lingeshughulikiwa ila aliwashauri wanachuo kufanya mazoezi mengine huku wakisubiria suala hilo kupatiwa ufumbuzi. Suala la uzembe wa walinzi limepigiwa kelele kwani kumekuwepo na wizi wa mara kwa mara na upotevu wa mali za wanafunzi kama vile Laptop na pesa taslimu nalo amesema lingefanyiwa kazi mapema.

Aidha, Mwanachuo mmoja alisikitishwa na mavazi ya wanachuo kwa sasa ambayo yanaondoa hadhi ya vitivo wanavyovisomea vya Uongozi na Sheria hasa wakina dada ambao wamefikia hatua ya kuvaa ngou zinazowaacha wazi sehemu kubwa ya miili yao hasa vifuani na kupendekeza kuwa uwekwe utaratibu maalumu wa mavazi rasmi (Dressing code) hasa muda wa vipindi ili kuweza kuleta hadhi yao na kuwatofautisha na watu wa mitaani.


No comments:

Post a Comment

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

IDADI YA WASOMAJI

RedEnvelope
. .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...