Saturday, November 3, 2012

BARAZA LA WANACHUO CHUO KIKUU MZUMBE LAFANYIKA

Mh. Amon Chakushemeire Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa  Chuo Kikuu  cha  Mzumbe  (MUSO)  akisoma hotuba  yake   kwenye Baraza la Wanachuo wa Chuo Kikuu Mzumbe, hotuba hiyo imewavutia wanachuo kwani imegusa matarajio yao kwa kiasi kikubwa na walionekana kufuatilia kwa makini na pia ilipongezwa na wanachuo hao ambao walipata nafasi ya kutoa maoni na kuuliza maswali. Kati ya mambo yaliyokonga mioyo ya wanachuo ni pamoja na suala la mabadiliko ya sheria za mitihani, Mikopo ya wanachuo kutoka bodi ya Mikopo hasa kwa kuwa walikuwa na shauku ya kujua hatima ya wanafunzi waliositishiwa mikopo yao kwa kupata "Supplementary", ambapo aliwahakikishia kuwa lilikuwa limeshashughulikiwa na wangeendelea kupata mikopo yao baada ya taratibu zote kukamilika, Aidha amewataka wanafunzi kuelewa mipaka ya Viongozi wao katika kufuatilia baadhi ya mambo na kuwaondoa wasiwasi wanachuo kwa kuwaomba wapuuze baadhi ya fikira potofu kutoka kwa watu wanaotaka umarufu wa kisiasa kwa madai kuwa Serikali haiwajali na kuwa haifuatilii matatizo yao na baadala yake kujenga utamaduni wa kufuatilia mambo muhimu kwa kupata taarifa kutoka sehemu husika (Viongozi wao) na si maneno yanayosemwa na wanafunzi wenzao. Akiongea kwa masikitiko makubwa alitoa mfano wa baadhi ya Habari ambayo ilikuwa ni ya uzushi na ambayo iliusikitisha Uongozi wa Chuo ya kuwa Chuo kilikuwa kikiweka pesa kwenye "fixed Account" zinazotoka Bodi ya Mikopo na kuwacheleweshea wanafunzi kwa makusudi, jambo ambalo halikuwa sahihi.

Wanachuo wakifuatilia kwa makini hotuba ya Rais wa Serikali ya Wanafunzi  Mzumbe (MUSO) katika Baraza la wanachuo  lililofanyika katika ukumbi wa National Assembly Hall maarufu kama NAH, Baraza hilo lilivunja rekodi ya mahudhurio ya miaka yote kwa kuhudhuliwa na wanachuo wengi. Wanachuo walionekana kuvutiwa na hotuba hiyo iliyovuta hisia zao, hasa pale alipogusia mambo mbalimbali ambayo serikali imefanikiwa kuyafanya kwa kipindi cha uongozi wake ikiwa ni kupata Sheria mpya za mitihani (Examination by-laws), Sheria ambazo zimekuwa ni   kiu kubwa ya wanafunzi wa Chuo kikuu cha Mzumbe, utatuzi wa tatizo la nyenzo za kufundishia (Audio systems na VLCDs) katika madarasa mbalimbali na upanuzi wa mawasiliano ya Internet (Wireless Extension) ili kukidhi mahitaji ya watumiaji wa mtandao. 

No comments:

Post a Comment

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

IDADI YA WASOMAJI

RedEnvelope
. .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...