Rais Baraka Obama amechaguliwa tena kuiongoza Marekani kwa mara nyingine. Ushindi huo umepelekea majonzi kwa wanachama wa Republican kwa kutoamini kilichotokea dakika 60 za mwisho zilizompa ushindi rais Baraka Obama. Hata hivyo mpinzani wake Mitt Ronney amempongeza Baraka Obama kwa ushindi huo na kukubali kuwa amemshinda na hana budi kufanya hivyo kwani ndiyo chaguo la wamarekani.
Kwa upande mwingine, ilikuwa ni furaha kubwa kwa wanachama wa Democrats kwa ushindi walioupata. Amewashukulu kwa kumchagua na kurudi Ikulu kwa mara nyingine, aidha amesema kuwa ushindi huo ni wa wamarekani wote bila kujali chama na majimbo wala waliomchagua au la na kusema kuwa kila mtu ana maoni yake binafsi na wamefanya maamuzi sahihi. Amewataka kutokusahau sera ya Marekani kuwa ni umoja, kazi na uzalendo ambayo imewafanya kuwa na mafanikio makubwa kuliko nchi yoyote duniani.
UONGOZI WA MUSO UNAMPONGEZA RAIS BARAKA OBAMA KWA KUCHAGULIWA TENA KUIONGOZA NCHI YA MAREKANI. TUNAMTAKIA MAFANIKIO MEMA KATIKA KIPINDI CHOTE CHA UONGOZI WAKE.
No comments:
Post a Comment