Katika picha (Kulia ni waziri wa Elimu, Mh. Vaileth Lusana na kushoto ni Naibu Waziri wa Elimu Mh. Joseph Kapyunka
Mkutano huo ulilenga kuwakaribisha viongozi wapya wa Wanafunzi na kuwaeleza kuhusu sheria mpya za mitihani, pia katika mkutano huo Viongozi wameshauliwa mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuyaelewa majukumu yao na kuyatekeleza kwa kufuata misingi ya kisheria.
Mh. Vaileth Lusana ambaye ni Waziri wa Elimu wa MUSO amewakumbusha Viongozi kujijengea utamaduni wa kutembelea mbao za matangazo ili kuweza kupata taarifa mbalimbali zitolewazo na Uongozi wa chuo. Aidha amewatahadharisha kutobweteka na baadala yake wasome kwa bidii ili kuwa mfano wa wanaowaongoza.
Amewataka kuwaelimisha wanafunzi wenzao juu ya sheria za Mitihani na kuzizingatia wawapo kwenye vyumba vya mitihani kwani kufanya hivyo kutawaepusha na matatizo yasiyo ya lazima.
|
No comments:
Post a Comment