Viongozi wa MUSO (Waliosimama nyuma) wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi.
Siku hiyo iliyopambwa na mada mbalimbali zilizomhusisha Baba wa Taifa Hayati Mwl. Nyerere katika harakati zake za kuupigania umoja wa Afrika na ule wa Afrika Mashariki mada ambazo zilitoa changamoto kwa hali ya sasa ambayo katika hali halisi umoja huo umeanza kutoweka kutokana na vita baridi zinazojitokeza katika nchi mbalimbali za Afrika na duniani kote zinazotokea kutokana na tofauti za kidini na siasa pia na Ufukara walionao raia wa nchi hizo unaohusishwa na Viongozi wasio waaminifu (Mafisadi).
Kwa upande mwingine imetolewa changamoto kwa vijana kutokuwa waoga katika soko la Afrika Mashariki na baadala yake kutumia fursa hiyo ili kujinufaisha kiuchumi, mfano wa fursa hizo ni pamoja na ile ya kutotozwa kodi kwa wafanyabishara wote wa bidhaa zinazozalishwa katika nchi hizo wanapokuwa wanasafirisha bidhaa zao kutoka nchi za jirani.
Akihitimisha Sherehe hiyo Mh. Prof. Daniel Mkude (Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Kikuu Mzumbe) ameomba watunga Sera za Elimu kufanya tathmini ya sera ya Elimu kuanzia shule ya Msingi ili kuwaandaa vijana kuwa na Elimu bora itakayowawezesha kupambana na changamoto mbalimbali za ajira na kuwa na umoja na hatimaye kujenga Umoja wa Nchi na Kimataifa.
|
No comments:
Post a Comment