Monday, October 22, 2012

Ndugu Amani (Mtaalamu wa ICT Mzumbe akifafanua juu ya matumizi  ya  Google  Apps  kwa  wanafunzi  wa  mwaka  wa  masomo 2012/2013 katika moja ya mafunzo yaliyotolewa katika mafunzo ya awali na kitengo cha Teknohama Mzumbe.

Mwalimu Ghasia (Mkurugenzi Mwandamizi wa Idara ya habari na Mawasiliano) akifundisha matumizi na umuhimu wa E-learning wanzafunzi wa  mwaka wa  masomo  2012/2013 katika mafunzo ya awali. 

Ndugu Albert (Naibu Waziri wa Habari na Mawasiliano akifafanua kuhusu  Blog  mpya  ya  MUSO  (Mzumbe  University Student  Organization) ambayo imelenga kutumika katika kupashana habari kati ya wanafunzi na Serikali yao juu ya matukio mbalimbali na kubadilishana mawazo pia kutoa maoni yao mbalimbali.

Bi. Domitila (Google Ambassador) akiwafundisha wanafunzi  matumizi  na  umuhimu wa  Google  Apps for  Education  Services.

Dr. Msabila (Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Mawasiliano)  Mzumbe  akitoa  mafunzo  ya  awali  kwa  wanafunzi wa  mwaka wa masomo 2012/2013 juu ya Teknohama na faida zake ambapo amefundisha matumizi ya ARIS na E-LEARNING. Wanafunzi walionekana kufurahia na kufuatilia kwa makini sana somo hilo kiasi cha kuomba liendelee kufundishwa mara kwa mara Chuoni. 

Wanafunzi wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa  mafunzo  ya  awali  ya  Habari na Mawasiliano  

No comments:

Post a Comment

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

IDADI YA WASOMAJI

RedEnvelope
. .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...