Friday, October 19, 2012

Porfesa Itika (Kaimu Makamu mkuu wa Chuo - DVC Accademic) akiwahutubia wanafunzi wa mwaka wa masomo  2012/2013  

Profesa Kamuzora (Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo - DVC Finance and  Administration)  akihutubia wanafunzi katika ukumbi wa NAH kwenye mafunzo ya awali kwa mwaka wa masomo 2012/2013

Wanafunzi wa mwaka wa masomo 2012/2013 wakifuatilia hotuba za Makaimu Wakuu wa Chuo  Kikuu  Mzumbe  kwenye  kipindi cha mafunzo ya awali (Orientation),  Makaimu wote wamewakaribisha wanafunzi na kuwapongeza kwa kuchaguliwa kujiunga na chuo Kikuu cha Mzumbe, aidha wamekumbushwa kutojihusisha na masuala ya siasa ya vyama na udini ndani ya Chuo.

Zoezi la Usajiri likiendelea katika ukumbi wa mihadhara (LT 1)  Kulia ni  Maofisa  wa  Idara  ya  fedha  Mzumbe  na  Kushoto Ni wanafunzi wapya wakiendelea na Usajiri. Zoezi hilo limepongezwa na Uongozi wa Chuo pia na wanafunzi kuwa limekuwa la kipekee na mafanikio ya hali ya juu. Aidha Serikali ya wanafunzi( MUSO), Idara ya Fedha na Vitivo wamepongezwa na Kaimu Mkuu wa Chuo kwa kufanikisha zoezi la Usajiri kwa ufanisi.

Msaidizi wa Mshauri Mkuu wa wanafunzi (kulia) na Naibu Waziri  wa  Elimu  (kushoto)  pamoja  na  wanafunzi  wakifuatilia kwa makini  hotuba za Makaimu Wakuu wa Chuo kikuu Mzumbe.

No comments:

Post a Comment

 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

IDADI YA WASOMAJI

RedEnvelope
. .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...