Na Albert Nzilolela
Baada ya mbwembwe nyingi za kampeni za Urais wa Serikali ya Wanafunzi Mzumbe (MUSO) zilizodumu kwa muda wa siku nane mfululizo hatimaye Rais mteule wa MUSO apatikana. Wagombea wa Urais waliokuwa kwenye kinyang'anyiro hicho cha kugombea nafasi hiyo kubwa ya Serikali ya wanafunzi ni pamoja na Lukiko Lukiko (Faculty of Law), Nicas Mahinda (School of Business) na Nicolas Magere (Faculty of Social Science).
Matokeo ya kula zilizopigwa yalikuwa kama ifuatavyo; Lukiko Lukiko ameongoza kwa kupata kula 977 akifuatiwa na Nicolas Magere aliyepata kula 850 nafasi ya tatu ilichukuliwa na Nicas Mahinda aliyejinyakulia kula 579. kwa matokeo hayo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi, Ndugu Mwashibanda Shibanda alimtangaza Lukiko Lukiko kuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi Mzumbe (MUSO) na Makamu wake atakuwa ni Bi Teddy Ladislaus kutoka Faculty of Science and Technology ambaye alikuwa ni mgombea mwenza katika kinyang'anyiro hicho cha kugombea. Wagombea wenza wengine waliofanikiwa kugombea nafasi hiyo ni pamoja na Jackline Daniel (School of Public Administration and Management) aliyekuwa mgombea mwenza wa Ndugu Magere na Frida Methusela (School of Public Administration and Management) mgombea mwenza wa Nicas Mahinda ambaye alikuwa amepewa nafasi kubwa ya kushinda nafasi hiyo lakini akaambulia nafasi ya mwisho.
Rais mteule anatarajiwa kuapishwa tarehe 25/01/2012 ambapo mara baada ya kiapo hicho ataanza rasmi majukumu ya kuitumikia Serikali ya Wanafunzi (MUSO).
No comments:
Post a Comment