Na Albert Nzilolela
Mwenyekiti wa Tume huru ya Uchaguzi MUSO, Ndugu Mwashibanda Lukas Shibanda amewatangazia Wagombea mbalimbali wenye nia ya kugombea nafasi za Uongozi wa Serikali ya Wanafunzi Mzumbe (MUSO) kuchukua fomu za kugombea nafasi hizo kuanzia tarehe 26/12/2012 hadi tarehe 28/12/2012. Muda wa kuchukua fomu utakuwa ni kuanzia saa 4:00 Aasubuhi hadi saa 10:00 jioni. Na kuwa mwisho wa kurejesha fomu hizo ni tarehe 29/12/2012. Nafasi zilizotangazwa kugombewa ni pamoja na Rais, Makamu wa Rais, Seneta, School Representatives (SRs) na Faculty Representatives (FRs).
Aidha, Mwenyekiti huyo ametoa tahadhari kwa wale wanaoanza kupiga kampeni ya kuwa muda wa kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria bado haujatangazwa na tume, na kuwa kuyafanya hivyo ni kinyume na sheria ya Uchaguzi kifungu cha sheria Na. 46 (2). Na kusema kuwa Mgombea yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufutiwa nafasi ya Ugombea katika nafasi husika.
No comments:
Post a Comment