Saturday, January 26, 2013

RAIS WA SERIKALI YA WANACHUO MZUMBE AAPISHWA



Na Albert Nzilolela

Rais mteule, Mh. Lukiko Lukiko wa Serikali ya wanafunzi Mzumbe (MUSO) ameapishwa katika ukumbi wa NAH na kufuatiwa na hafla ya kumpongeza iliyofanyika katika hotel ya Lumumba Complex Mzumbe. Kabla ya kuapishwa, alitanguliwa na hotuba ya Rais anayemaliza kipindi chake cha uongozi na Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi. Mgeni Rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliyewakilishwa na Afisa Utumishi wa Mkoa Ndugu Elias Andrew.

Rais anayemaliza muda wake Mh. Amon Chakushemeire amewashukulu sana wanachuo kwa kumuamini na kumchagua kuiongoza Serikali ya wanachuo (MUSO). Katika hotuba yake ameushukulu uongozi wa Chuo pamoja na Baraza la mawaziri na Bunge la wanachuo kwa kumpa ushirikiano wa hali juu kwani anaamini kuwa ushirikiano huo ndiyo umepelekea yeye kumaliza muda wake kwa heshima kubwa na mafanikio makubwa. Pia alionesha kusikitishwa na dhana ya wanachuo kudhani kuwa wana ufahamu wa kila jambo kwa kutojali kusoma hata matangazo yanayowahusu suala linalopelekea kutokuhudhuria semina na midahalo mbalimbali inayofanyika chuoni. Lakini pia amekiri kuwa ni kazi ngumu sana kuwaongoza wasomi.

Mwenyekiti wa tume amezungumzia changamoto mbalimbali zinazoikumba tume ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na bajeti finyu kwa ajili ya kuendeshea shughuli za uchaguzi, upatikanaji wa taarifa za wanafunzi kwa muda, wanafunzi  kutokuwa na hulka ya kusoma matangazo suala ambalo lilipelekea wagombea wengi kurejesha fomu za kuteuliwa kuwa wagombea kwa kuchelewa, upatikanaji wa mwenyekiti wa tume kwa kigezo cha kuwa mtu mwenye uelewa au taaluma katika masuala ya sheria kuwa kinawanyima haki wanachuo wengine kugombea nafasi hiyo.

Baada ya hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Rais mteule na makamu wake Mh. Teddy Ladislaus wameapishwa na kufuatiwa na hotuba ya Rais huyo, Mh. Lukiko Lukiko. Katika hotuba yake amewashukulu wanachuo kwa kumpa nafasi hiyo kubwa ya kuiongoza serikali ya MUSO. Aidha, Rais Lukiko amesema kuwa anaamini kuwa njia sahihi ya kufanikisha jambo lolote ni kwa njia ya majadiliano na ushirikiano.

Aidha Rais Lukiko amewahakikishia wanachuo waliofika katika hafla hiyo ya kuapishwa kwake kuwa angejitahidi kuweka mazingira bora ya kuwafanya wanachuo wapate mafanikio mazuri kitaaluma. Amegusia mambo mbalimbali ya kijamii kama vile unyanyapaaji wa waathirika wa UKIMWI, Rushwa, Chuki zinazotokana tofauti za kisiasa pamoja na mifumko ya bei za vitu. Ameahidi kuandaa midahalo mbalimbali ya majadiliano ili kutoa elimu juu ya changamoto hizo ambazo ni vikwazo vya maendeleo pia ametoa wito kwa wasomi kutumia elimu yao kusaidia jamii zinazowazunguka hasa watu wa vijijini.
Hotuba ya Rais Lukiko imefuatiwa na hotuba ya Profesa Kamuzora (Kaimu Makamu mkuu wa Chuo) ameipongeza serikali iliyomaliza muda wake kwa umahili mkubwa na ufanisi katika utendaji kazi wake na kumaliza muda wake pasipokuwa na matatizo yoyote na kukili kuwa hakuamini kuwa muda wa uongozi ulikuwa umeisha kwani aliona kuwa ni muda mfupi sana kwa kusema kuwa ameona kama siku zilikuwa zimekimbia sana kwa upande mwingine amempongeza Rais aliyekuwa anamalizia muda wake Mh. Amoni Chakushemeire kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TAHLISO na kusema kuwa hiyo inadhihirisha kuwa ni Kiongozi bora na mtu anayekubalika si ndani ya chuo bali hata nje ya mipaka ya chuo pia amempongeza Rais mpya Mh. Lukiko Lukiko kwa kuaminiwa na kuchaguliwa na wanachuo na kusema kuwa amechaguliwa kuwaongoza wanachuo hivyo hana budi kuwatumikia kwa bidii. Amewashauri wanafunzi kujenga tabia ya kutumia “website” ya chuo na “blog” ya MUSO kupata taarifa mbalimbali zinazohusiana na chuo kwani suala la matumizi ya mbao kwa ajili ya matangazo litasitishwa mara moja hivi karibuni.

Baada ya hafla hiyo ya kuapishwa lilifuatia tukio ya sherehe ya kumpongeza iliyofanyikia katika hoteli ya Lumumba Complex iliyoko Mzumbe. Katika sherehe hiyo wazazi walipata fursa ya kumpongeza Rais Lukiko. Baba mzazi, Ndugu Ilvin Mgeta amempongeza mwanae na keahidi kuwa atampa ushirikiano katika kipindi chake cha Uongozi, pamoja na pongezi hizo amemtahadharisha Rais Lukiko kuwa kazi aliyopewa ni kubwa na ina majukumu makubwa hivyo amemtaka kutumia muda wake vizuri ili kuhakikisha haporomoki kimasomo.

MATUKIO KATIKA PICHA


Mh. LUKIKO LUKIKO (RAIS MTEULE WA SERIKALI YA WANAFUNZI)  AKIAPISHWA

Mh. TEDDY LADISLAUS (Makamu wa Rais wa Serikali ya wanachuo MUSO)  AKIAPISHWA

Mh. Lukiko Lukio Rais Mteule (kulia) akiwa na Mh. Amon Chakushemeire (kushoto) Rais anayemaliza muhula wake
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Ndugu Mwashibanda Shibanda akitoa tathmini ya Uchaguzi wa mwaka 2013

Mama mzazi wa Rais Lukiko, Mrs. Yusta Mgeta akimpongeza mwanae kwa kuchaguliwa 

Baba mzazi wa Rais Lukiko, Ndugu Ilvin Mgeta akimpongeza mwanae katika sherehe ya kumpongeza Rais iliyofanyika Lumumba complex. 

Baadhi ya Viongozi wa MUSO (mbele) na wanachuo wakishuhudia Rais wa Serikali ya MUSO pindi akiapishwa

Viongozi wa MUSO wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali ya kuapishwa kwa Rais Lukiko.


Sunday, January 13, 2013

HATIMAYE RAIS WA MUSO APATIKANA


Na Albert Nzilolela

Baada ya mbwembwe nyingi za kampeni za Urais wa Serikali ya Wanafunzi Mzumbe (MUSO) zilizodumu kwa muda wa siku nane mfululizo hatimaye Rais mteule wa MUSO apatikana. Wagombea wa Urais waliokuwa kwenye kinyang'anyiro hicho cha kugombea nafasi hiyo kubwa ya Serikali ya wanafunzi ni pamoja na Lukiko Lukiko (Faculty of Law), Nicas Mahinda (School of Business) na Nicolas Magere (Faculty of Social Science).

Matokeo ya kula zilizopigwa yalikuwa kama ifuatavyo; Lukiko Lukiko ameongoza kwa kupata kula 977 akifuatiwa na Nicolas Magere aliyepata kula 850 nafasi ya tatu ilichukuliwa na Nicas Mahinda aliyejinyakulia kula 579. kwa matokeo hayo Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi, Ndugu Mwashibanda Shibanda alimtangaza Lukiko Lukiko kuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi Mzumbe (MUSO) na Makamu wake atakuwa ni Bi Teddy Ladislaus kutoka Faculty of Science and Technology ambaye alikuwa ni mgombea mwenza katika kinyang'anyiro hicho cha kugombea. Wagombea wenza wengine waliofanikiwa kugombea nafasi hiyo ni pamoja na Jackline Daniel (School of Public Administration and Management) aliyekuwa mgombea mwenza wa Ndugu Magere na Frida Methusela (School of Public Administration and Management) mgombea mwenza wa Nicas Mahinda ambaye alikuwa amepewa nafasi kubwa ya kushinda nafasi hiyo lakini akaambulia nafasi ya mwisho.

Rais mteule anatarajiwa kuapishwa tarehe 25/01/2012 ambapo mara baada ya kiapo hicho ataanza rasmi majukumu ya kuitumikia Serikali ya Wanafunzi (MUSO).
 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

IDADI YA WASOMAJI

RedEnvelope
. .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...